Lango:Cote d'Ivoire
Milango ya Wikipedia: Sanaa · Utamaduni · Jiografia · Afya · Historia · Hisabati · Sayansi · Falsafa · Dini · Jamii · Teknolojia Iliwahi kuwa kati ya nchi tajiri zaidi za Afrika lakini tangu mwaka 2002 uchumi na hali ya maisha zimeharibika kutokana na vita ya wenyewe kwa wenyewe. Alpha Blondy (jina la kulizaliwa: Seydou Koné; * Dimbokoro, Côte d'Ivoire, 1 Januari 1953), ni mwanamuziki wa Reggae na msanii anayerekodi nyimbo zake nyingi kimataifa. Alpha Blondy mara nyingi huimba kwa lugha ya Kidioula ambayo ndio lugha yake ya taifa huku akichanganya Kifaransa na Kiingereza, lakini pia wakati mwingine huimba kwa Kiarabu au Kiyahudi. Mashairi yake yanamaanisha siasa kali yenye mwelekeo na uchangamfu. Alpha ni mtoto wa kwanza katika familia ya watoto tisa, Jina la kuzaliwa ni Seydou Kone amezaliwa mjini Dimbokro mnamo 1953. Alilelewa na bibi yake mzaa mama. Mnamo mwaka 1962, Alpha Blondy alikwenda kukaa na baba yake aliyekuwa anaishi mjini Odienne, Ambapo alikaa kwa muda wa miaka kumi, Baadae akijiunga na shule ya Sainte Elisabeth high school, na kujishughulisha na makundi ya wanafunzi ya Ivory Coast. Hapo ndipo alipo unda bendi. Ingawaje, Upenzi huu uliathiri masomo yake na baadae Blondy alikufukuzwa shule kutokana na maudhulio mabovu shuleni.
Serikali ya Côte d'Ivoire (Ivory Coast) inachukua nafasi katika mfumo wa uwakilishi wa uraisi katika jamhuri ya kidemokrasia, ambapo Rais wa Cote d'Ivoire ni mkuu wa nchi na vilevile ni kiongozi wa serikali, na inafuata mfumo wa vyama vingi. Nguvu ya kiutendaji hutimizwa na serikali tu. Suala la utunzi wa sheria hutekelezwa kwa njia ya serikali yenyewe au bunge. Mji mkuu rasmi tangu 1983 ni Yamoussoukro; hata hivyo, Abidjan unabaki kuwa kitovu cha utawala. Nchi nyingi huweka balozi zao mjini Abidjan, ijapokuwa baadhi yao (ikiwa ni pamoja na Uingereza) wamefunga harakati zao kwa sababu ya fujo zinaoendelea na ushambuliaji dhidi ya Wazungu. Wakazi wanaendelea kupata shida kwa kufuatia vita ya wenyewe kwa wenyewe inayoendelea.
|